Social

Friday, February 24, 2017

Wema: Sijasukumwa na hasira, natafuta demokrasia



Dar es Salaam. Siku moja baada ya kuhamia Chadema, msanii maarufu nchini wa fani ya uigizaji wa filamu, Wema Sepetu (28) amefunguka na kusema amefanya maamuzi ya kibinadamu wala hajasukumwa na hasira.
Akikabidhiwa kadi ya Chadema leo (Ijumaa), nyumbani kwa mama yake, Sinza jijini hapa, Wema amesema sasa ameingia kwenye mapambano.

“Kswa yaliyonikuta nilijiuliza wapi nilikosea, nilijitoa kuitumikia CCM kwa utu wangu wote, uamuzi wangu sijauchukua kwa hasira bali natafuta demokrasia,”amesema Wema.

0 comments:

Post a Comment