Social

Monday, February 27, 2017

Wanajihad wamkata kichwa raia wa Ujerumani



Wapiganaji wa Kiislamu nchini Ufilipino wamechapisha kanda ya video inayoonyesha mateka mmoja wa Ujerumani akikatwa kichwa.
Jurgen Kanther alitekwa nyara katika jahazi lake pwani ya Malaysia jimbo la Sabah mnamo mwez Novemba.
Mwili wa mtu aliyekuwa naye baadaye ulipatikana katika mashua hiyo.
Siku ya mwisho ya kulipa fidia ya dola 483,000 ilikamilika siku ya Jumapili.
Bw Kantner mwenye umri wa miaka 70 na bi Merz walikuwa wamewahi kutekwa nyara awali.
Walizuiliwa kwa siku 52 mwaka 2008 na maharamia wa Kisomali na waliachiliwa huru baada ya kikombozi kutolewa.

Mjumbe wa serikali Jesus Dureza alithibitisha mauaji hayo.
Hadi wakati wa mwisho sekta tofauti ikiwemo jeshi zilishindwa kuokoa maisha yake.
''Sote tulijaribu uwezo wetu lakini hatukufanikiwa'',alisema.

Mjumbe wa serikali Jesus Dureza alithibitisha mauaji hayo.
Hadi wakati wa mwisho sekta tofauti ikiwemo jeshi zilishindwa kuokoa maisha yake.
''Sote tulijaribu uwezo wetu lakini hatukufanikiwa'',alisema.

0 comments:

Post a Comment