Dar es
Salaam. Hii ni baada ya mrembo wa Tanzania wa mwaka 2006, Wema Sepetu
kujitokeza mahakamani kumsindikiza Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
katika kesi ambayo mbunge huyo wa Hai amefungua dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam, Paul Makonda, Kamanda wa Polisi Kanda ya Dar es Salaam, Simon Siro na
sasa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Jana, Wema
alikuwa Mahakama Kuu akionekana mwenye furaha na wakati fulani akinyoosha
vidole viwili, alama inayotumiwa na Chadema. Alikuwa amekaa karibu na Mbowe,
huku pembeni akionekana Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya.
Wakati
Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alipojitokeza juzi kumtetea msanii
huyo, ilionekana ni jukumu lake la kawaida la kiwakili lakini jana ndipo ilipodhihiri
siri iliyokuwa ndani.
Picha za
Wema zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii na muda mfupi baadaye ofisa habari
wa Chadema, Tumaini Makene alituma ujumbe ulioarifu kuwa Mbowe angeongea na
umma kupitia vyombo vya habari.
0 comments:
Post a Comment