Dar es Salaam. Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema) Tundu Lissu amekamatwa nyumbani kwake Dodoma leo (Alhamisi) na kupelekwa katika ofisi ya kamanda wa polisi wa mkoa huo.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa polisi wa mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa amesema ni kweli amekatawa na anasafirishwa kwenda Dar es Salaam kwa madai kuwa ameruka dhamana.
Lissu ambaye pia ni wakili maarufu nchini, anagombea nafasi ya urais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).
0 comments:
Post a Comment