Social

Monday, March 27, 2017

Wasichana waliovalia suruali za kubana wazuiwa kupanda ndege ya United Airlines Marekani


Ndege za United Airlines

Shirika la ndege la United Airlines nchini Marekani limeshutumiwa sana baada ya kudaiwa kuwazuiwa wasichana wawili waliokuwa wamevalia suruali ndefu za kubana kuabiri ndege hiyo.
Kisa hicho kilitokea kwenye safari ya ndege iliyokuwa ikitokea Denver kuelekea Minneapolis Jumapili asubuhi, mwanaharakati Shannon Watts amesema.
Shirika la United limesema wasichana hao walikuwa wanasafiria hati maalum, ambayo hutumiwa na wafanyakazi wa shirika la ndege na wageni wao.
United wamesema huwa kuna kanuni za mavazi kwa wanaotumia hati hiyo kusafiria.
Shirika hilo limefafanua kwamba abiria wa kawaida, ambao wanalipia tiketi zao, wako huru kuvalia mavazi yao ya kubana.
Hati hiyo maalum ya kusafiria ya United huwawezesha walio na hati hiyo kusafiri kwa ndege bila malipo au kwa tiketi za bei nafuu sana.
Kanuni za mavazi kwa wanaotumia hati hiyo hueleza kuwa hawafai kuvalia mavazi ya kubana, iwe ni blauzi za lycra/spandex, suruali ndefu au rinda.
Aidha, hawaruhusiwi kuvalia mavazi yanayoanika vitovu vyao au minisketi.
Mwanaharakati Shannon Watts ameandika kwenye Twitter kwamba kisa hicho kiliathiri wasichana karibu watano waliokuwa wakitaka kuabiri ndege uwanja wa ndege wa Denver.
Alisema wakala mmoja wa United alijaribu kuwashurutisha wasichana hao, mmoja wa umri wa miaka 10, kubadilisha mavazi yao na kuvalia marinda badala ya long'i hizo za kubana.
Alisema wasichana watatu kati ya hao waliruhusiwa kuabiri ndege baada ya kukubali kuvalia marinda, lakini hao wengine wawili walizuiwa kuabiri ndege.

Tweet from Shannon Watts reads: 1) 3 girls inspected for wearing perfectly acceptable leggings. 2 not allowed to board. I don't care what kind of passengers they were.

Alishutumu shirika hilo, na kuuliza: "Ni wakati gani United waligeuka na kuwa polisi wa kuamua kuhusu mavazi?"

Tweet from Shannon Watts reads: 2) This behavior is sexist and sexualizes young girls. Not to mention that the families were mortified and inconveninced.
Tweet from Shannon Watts reads: 3) As the mother of 4 daughters who live and travel in yoga pants, I'd like to know how many boys @United has penalized for the same reason.
Tweet from Shannon Watts reads: 4) Their father, who was allowed to board with no issue, was wearing shorts.

United baadaye walijibu kwenye Twitter wakisema wenye hati hizo maalum hutakiwa kufuata kanuni maalum za mavazi.

Tweet from United reads: We appreciate you being our eyes and ears. The customers this morning were United pass travellers

0 comments:

Post a Comment