Social

Sunday, March 26, 2017

Wanasiasa wajadili hatima ya Nape kisiasa



Wanasiasa, wakiwamo wa vyama vya upinzani wamezungumzia hatima ya kisiasa ya aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye huku wakimshauri kurejea jimboni kwake kujiimarisha na kutokata tamaa.
Ushauri huo umekuja siku chache baada ya Rais John Magufuli kumwondoa katika nafasi hiyo.
Alhamisi iliyopita, Rais Magufuli alimteua Dk Harrison Mwakyembe kuchukua nafasi ya Nape na kumteua Profesa Palagamba Kabudi kuwa Waziri wa Katiba na Sheria kujaza nafasi ya Dk Mwakyembe.
Dalili za Nape kuingia katika msukosuko wa kiutawala zilianza Februari baada ya kujitokeza hadharani na kutoa angalizo kuhusu baadhi ya wasanii ambao walikuwa wametajwa kuhusika na matumizi au biashara ya dawa za kulevya.
Akiwa waziri anayewasimamia, alitaka busara itumike katika mapambano hayo akibainisha kwamba kinyume chake itakuwa ni kuchafua majina na umaarufu wa wasanii hao uliojengwa kwa muda mrefu ikiwa itabainika kuwa hawahusiki.
Pia ilionekana kama amepishana na mamlaka za juu jinsi alivyoshughulikia suala la kuvamiwa kwa kituo cha Clouds Media Group.

0 comments:

Post a Comment