Dar es Salaam. Habari zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa mkutano wa Mbunge wa Mtama(CCM) Nape Nnauye umezuiwa kufanyika katika hoteli ya Protea.
Taarifa hizo ambazo hata hivyo hazijathibitishwa zimeeleza kuwa Kamanda wa Polisi wa Kinondoni Suzana Kaganda amepiga simu hotelini na kuzuia mkutano huo.
Hata hivyo baadhi ya waandishi waliokuwapo eneo hilo walizungumza na Nape kwenye simu ambaye aliwaahidi kuwa atafika kwenye eneo hilo baada ya muda mfupi na kuzungumza nao.
0 comments:
Post a Comment