Social

Sunday, March 12, 2017

Mashabiki wamshukia Lwandamina



Dar es Salaam. Yanga imesononesha mashabiki wake huku ikijiweka katika mazingira magumu ya kufuzu kwa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Zanaco ya Zambia.
Ugumu wa matokeo hayo ni kwamba, Zanaco watataka kushinda ama kutoka suluhu huku salama ya Yanga ni sare ya 2-2 au ushindi.
Hata hivyo, timu itakayopoteza mchezo wa marudiano, itashuka hadi michuano ya Kombe la Shirikisho. Timu hizo zinarudiana kati ya Machi 17 na 19 mjini Lusaka, Zambia.
Mabadiliko Yanga
Bao la Simon Msuva la dakika ya 37 liliwafanya Yanga kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa uongozi wa bao 1-0.
Kipindi cha pili kilikuwa bora zaidi kwa Zanaco walioonekana kutaka kurudisha bao na kufanya mashambulizi mengi bila umakini.

0 comments:

Post a Comment