Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Augustine Mahiga amesema Serikali za Tanzania na Afrika Kusini zimeweka mikakati ya kuongeza maeneo ya ushirikiano, hususan katika biashara na uwekezaji.
Balozi Mahiga amesema hayo leo (Alhamisi) asubuhi alipotoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa mawaziri wa kamisheni ya pamoja ya kitaifa kati ya Tanzania na Afrika Kusini uliofanyika jijini hapa.
Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Kusini, Maite Nkoana -Mashabane ameeleza umuhimu wa kukuza uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya mataifa hayo mawili ili kuwaletea maendeleo wananchi wa mataifa yote.
Pia, ametumia fursa hiyo kutoa rambirambi kwa Tanzania kwa vifo vya watoto 32, walimu wawili na dereva mmoja wa Shule ya Lucky Vincent vilivyotokea wiki iliyopita mkoani Arusha. Amesema ajali imepunguza nguvu kazi na wataalamu wa kizazi kijacho.
0 comments:
Post a Comment