Social

Wednesday, April 5, 2017

Waziri wa Afya amteua Lwezimula Mkurugenzi wa MOI


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,

 Dar es Salaam. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amemteua Dk Respicious Lwezimula Boniface kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI).
 Awali nafasi hiyo ilikuwa ikikaimiwa na Dk Othman Kiloloma.
Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa wizara, Nsachris Mwamaja ilisema, kabla ya uteuzi huo Dk Respicious Lwezimula alikuwa daktari bingwa katika Taasisi hiyo na kwamba uteuzi huo unaanza leo Aprili 5.
Ummy alisema nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa MOI ilikuwa wazi tangu mwaka 2014 baada ya aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji kustaafu kwa mujibu wa sheria.

0 comments:

Post a Comment