Zanzibar. Wajumbe wa Baraza Kuu la Chama Cha Wananchi (CUF) wanamuunga mkono Katibu Mkuu wa chama hicvho, Maalim Seif Sharif Hamad, wameanza kuuingia makao makuu kwa ajili ya kikao cha baraza hilo kinachofanyika leo Vuga, Zanzibar.
Kikao hicho, ambacho mwenyekit wa taifa anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, profesa Ibrahim Lipumba, amesema kuwa hakitambui, kinatarajiwa kuendeshwa na Maalim Seif.
Baraza hilo kuu linatarajiwa kujadili mambo mbalimbali na kuweka msimamo kuhusiana na kufukuzwa kwa wabunge wanane wa viti maalum hivi karibuni.
Imedaiwa kwamba kikao hicho kimeitishwa kwa kufuata masharti ya Katiba ya CUF ya mwaka 1992 (Toleo la 2014), kifungu cha 80 (1), ambacho kinaipa uwezo Kamati ya Utendaji ya Taifa ya Chama kuitisha kikao cha dharura cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa
0 comments:
Post a Comment